X

Vous n'êtes pas connecté

Rubriques :

  - MSUMBANEWS.CO.TZ - A La Une - 15/Jul 06:59

TBA YAWASHUKURU WANANCHI, YAAHIDI MABORESHO ZAIDI YA HUDUMA

  Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Daudi Kondoro, ametoa shukrani kwa wananchi wote waliotembelea Banda la TBA katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yaliyofanyika katika Viwanja vya Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 28 hadi Julai 13, 2025. Akizungumza mara baada ya kufungwa kwa maonesho hayo, Arch. Kondoro amesema TBA inawashukuru wananchi, viongozi wa serikali na wadau mbalimbali waliotembelea banda hilo, kujionea miradi mbalimbali inayotekelezwa na wakala huo na kutoa maoni yenye lengo la kuboresha huduma. "Tunawashukuru kwa dhati watu wote waliotembelea Banda letu, kuona miradi yetu na kutoa maoni muhimu ambayo tumeanza kuyafanyia kazi kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma tunazotoa kwa umma," amesema Kondoro. Aidha, ametoa pongezi kwa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kwa kuratibu vizuri maonesho hayo na kuwezesha taasisi mbalimbali, ikiwemo TBA, kuwafikia wananchi. Mtendaji Mkuu huyo amebainisha kuwa maoni yote yaliyokusanywa kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali wakati wa maonesho hayo, pamoja na taarifa kuhusu huduma zinazotolewa na wakala huo, yatatolewa kupitia tovuti mpya ya TBA ambayo inatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni. Katika hatua nyingine, Arch. Kondoro ameeleza mafanikio mengine yaliyopatikana kupitia maonesho hayo, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa nia ya ushirikiano baina ya TBA na wawekezaji mbalimbali wanaotaka kushirikiana katika miradi ya ubia. Kuhusu maendeleo ya mradi wa nyumba za makazi katika eneo la Bunju, jijini Dar es Salaam, unaowahusisha watumishi wa umma, Mtendaji Mkuu huyo amesisitiza kuwa mradi huo haujatelekezwa. "Napenda kuwatoa hofu wakazi wa mradi wetu wa Bunju kuwa, mradi ule bado ni wa kwetu na mwezi Agosti mwaka huu tutakutana nao kujadili namna ya kuendeleza maboresho ya mradi huo," amesema Kondoro. Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuwakutanisha wazalishaji wa bidhaa na huduma kutoka ndani na nje ya nchi, na huratibiwa na TANTRADE.

Articles similaires

TBA YAWASHUKURU WANANCHI, YAAHIDI MABORESHO ZAIDI YA HUDUMA

msumbanews.co.tz - 15/Jul 06:59

  Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Daudi Kondoro, ametoa shukrani kwa wananchi wote waliotembelea Banda la TBA katika...

MWAIPAJA: TUTAENDELEA KUTOA ELIMU KWENYE MAJUKWAA MENGINE BAADA YA SABASABA

msumbanews.co.tz - 14/Jul 04:49

 Na. Peter Haule na Joseph Mahumi,WF, Dar es Salaam Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja amewataka...

MWAIPAJA: TUTAENDELEA KUTOA ELIMU KWENYE MAJUKWAA MENGINE BAADA YA SABASABA

msumbanews.co.tz - 14/Jul 04:49

 Na. Peter Haule na Joseph Mahumi,WF, Dar es Salaam Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja amewataka...

DKT.YONAZI AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU MAONESHO SABASABA

msumbanews.co.tz - 18/Jul 13:20

 Na Mwandishi wetu- DodomaKatibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya...

DKT.YONAZI AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU MAONESHO SABASABA

msumbanews.co.tz - 18/Jul 13:20

 Na Mwandishi wetu- DodomaKatibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya...

“LENGO KUU LA KUSHIRIKI MAONESHO HAYA NI KUTOA ELIMU KWA UMMA” – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

msumbanews.co.tz - 10/Jul 18:08

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amefanya ziara ya kutembelea maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea...

“LENGO KUU LA KUSHIRIKI MAONESHO HAYA NI KUTOA ELIMU KWA UMMA” – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

msumbanews.co.tz - 10/Jul 18:08

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amefanya ziara ya kutembelea maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea...

Dkt. Biteko- Sekta ya Nishati Ni Uti wa Mgongo wa Maendeleo ya Viwanda Nchini

msumbanews.co.tz - 11/Jul 05:51

 SERIKALI ya Tanzania imeendelea kuchukua hatua thabiti za kuboresha upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ya viwanda...

BILIONI MBILI KUKAMILISHA UJENZI WA BARABARA ZA TARURA JIJI LA ARUSHA

msumbanews.co.tz - 12/Jul 06:10

Wakala wa Barabra za mijini na Vijini TARURA  wanatarijia zaidi ya bilioni mbili kukamilisha Ujenzi wa Barabara ya TCA Levolisi,CCM,...

WAZIRI MAVUNDE AKAGUA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA NANE LA MAFUNZO YA UONGEZAJI THAMANI MADINI VITO

msumbanews.co.tz - 22/Jul 15:26

  ▪️Bilioni 33 kukutumika kukamilisha Jengo la ghorofa pacha-TGC Arusha▪️Biashara ya madini kufanyika kwenye Jengo▪️Ni mkakati wa...

Les derniers communiqués

  • Aucun élément