X

Vous n'êtes pas connecté

Rubriques :

  - MSUMBANEWS.CO.TZ - A La Une - 18/Jul 13:20

DKT.YONAZI AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU MAONESHO SABASABA

 Na Mwandishi wetu- DodomaKatibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kwa maendeleo ya Taifa.Dkt. Yonazi ameyasema hayo leo tarehe 18 Julai, 2025 Ofisini kwake jijini Dodoma akikabidhiwa tuzo na  Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw. Conrad Milinga iliyotolewa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati akifungua Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025.Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu kupokea tuzo kumeongeza motisha katika ushiriki wa maonesho yajayo makubwa ya Kimataifa ya Sabasaba  na kutambua mchango wa Ofisi hiyo iliyoutoa kwa wananchi katika kipindi chote cha maonesho hayo na kutambua huduma ianayotolewa kwa wananchi.“Ofisi ya Waziri Mkuu imefurahi sana kupokea tuzo hii kama ishara ya kutambua ushiriki wetu na mchango ambao Ofisi yetu inatoa kwa wananchi hivyo tunaamini ushiriki wetu unaofuata utakuwa wa viwango vya juu sana,” Alisema Dkt. Yonazi.Pia  aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazofanya chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) ambayo ndio mratibu wa Maonesho kwa  kuhakikisha maonesho hayo yanaleta tija na mageuzi makubwa katika sekta ya kiuchumi kwa wananchi na Kimataifa.“Tunazishukuru sana Taasisi mbalimbali ambazo tumeshirikiana nazo na viongozi ambao wameendelea kutupa maelekezo yaliyowezesha kufanya vizuri katika maonesho hayo na tunaamini kwamba tutaendelea kuwa washindi au hata washindi wa jumla,”Alishukuru.Ikumbukwe Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025 yalifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi tarehe 07 Julai, 2025 na kufungwa na Waziri Mkuu Mhe.  Kassim Majaliwa  katika viwanja vya maonesho Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 13, 2025.

Articles similaires

DKT.YONAZI AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU MAONESHO SABASABA

msumbanews.co.tz - 18/Jul 13:20

 Na Mwandishi wetu- DodomaKatibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya...

WASHIRIKA WA MAENDELEO KUCHANGIA SH. BILIONI 161 MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

msumbanews.co.tz - 19/Jul 06:26

 Na. Peter Haule, WF, Dar es SalaamSerikali ya Tanzania na washirika wa Maendeleo wanaochangia Mfuko wa Afya wa Pamoja (Health Basket Fund),...

WASHIRIKA WA MAENDELEO KUCHANGIA SH. BILIONI 161 MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

msumbanews.co.tz - 19/Jul 06:26

 Na. Peter Haule, WF, Dar es SalaamSerikali ya Tanzania na washirika wa Maendeleo wanaochangia Mfuko wa Afya wa Pamoja (Health Basket Fund),...

DKT. YONAZI AIPONGEZA SERIKALI MAGEUZI SEKTA YA KILIMO

msumbanews.co.tz - 16/Jul 12:00

 Na Mwandishi wetu- MorogoroSerikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imepongezwa kwa kuendelea kufanya mageuzi...

DKT. YONAZI AIPONGEZA SERIKALI MAGEUZI SEKTA YA KILIMO

msumbanews.co.tz - 16/Jul 12:00

 Na Mwandishi wetu- MorogoroSerikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imepongezwa kwa kuendelea kufanya mageuzi...

WAZIRI LUKUVI ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA 2025

msumbanews.co.tz - 16/Jul 13:46

 Na Mwandishi wetu- DODOMAWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. William Lukuvi amefanya ukaguzi wa maandalizi ya...

WIZARA ZINGINE ZIIGE MFANO WA WIZARA YA AFYA KUHAMIA MTUMBA- LUKUVI

msumbanews.co.tz - 23/Jul 17:55

 Na WAF - Dodoma Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi ameipongeza Wizara ya Afya kwa kuchukua uamuzi wa...

DKT. BITEKO ATOA WITO VYOMBO VYA HABARI KUELIMISHA JAMII KUHUSU MASHUJAA

msumbanews.co.tz - 24/Jul 10:10

 📌Rais Samia mgeni rasmi Maadhimisho ya Mashujaa kesho📌Atoa wito kwa wananchi kushiriki Maadhimisho ya MashujaaNa Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na...

DKT. BITEKO ATOA WITO VYOMBO VYA HABARI KUELIMISHA JAMII KUHUSU MASHUJAA

msumbanews.co.tz - 24/Jul 10:10

 📌Rais Samia mgeni rasmi Maadhimisho ya Mashujaa kesho📌Atoa wito kwa wananchi kushiriki Maadhimisho ya MashujaaNa Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na...

TANZANIA NA UTURUKI ZAWEKA LENGO KUBWA LA KIBIASHARA

msumbanews.co.tz - 23/Jul 18:01

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,na Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK,wakibadilishana Mkataba mara...

Les derniers communiqués

  • Aucun élément