X

Vous n'êtes pas connecté

Rubriques :

  - MSUMBANEWS.CO.TZ - A La Une - 23/Jul 18:01

TANZANIA NA UTURUKI ZAWEKA LENGO KUBWA LA KIBIASHARA

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,na Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK,wakibadilishana Mkataba mara baada ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki hafla iliyofanyika leo Julai 23,2025 jijini jijini Dar es Salaam. Na.Mwandishi Wetu SERIKALI ya Tanzania imeweka malengo makubwa ya kibiashara kwa kushirikiana na Uturuki, ikilenga kufikia thamani ya biashara ya Dola za Kimarekani bilioni 1. Hii ni sehemu ya jitihada za kuimarisha uchumi wa nchi kupitia diplomasia ya kiuchumi na kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa za Tanzania katika soko la Uturuki. Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,amesema kuwa ushirikiano huo unalenga kuzalisha bidhaa bora na kukuza sekta ya viwanda, kilimo na madini kwa masoko ya kimataifa. “Kupitia timu ya wataalamu na ushirikishwaji wa sekta binafsi, tutashirikiana katika biashara kama lango kuu la fursa,” amesema Dkt. Jafo. Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2024, biashara kati ya Tanzania na Uturuki ilikuwa Dola milioni 284, ambapo Uturuki iliuza bidhaa zenye thamani ya Dola milioni 217 kwa Tanzania, ikionesha fursa kubwa bado hazijatumika kikamilifu. Waziri Jafo ameeleza kuwa mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na Uturuki yameimarika kwa kasi, hasa baada ya kufunguliwa kwa balozi za nchi hizo mwaka 2009 na 2017 mtawalia. Amesema kuwa ziara za viongozi wakuu wa mataifa haya, ikiwemo ile ya Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan nchini Tanzania na ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Uturuki mwaka 2024, zimekuwa kichocheo kikubwa cha ushirikiano huu. Vilevile,amesema kuwa makampuni ya Kituruki yamekuwa sehemu ya miradi mikubwa ya maendeleo nchini, kama vile ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), ambayo imeleta ajira na fursa mpya kwa Watanzania. “Makampuni ya Uturuki, hasa kwenye SGR, yameweza kufanya biashara ambayo italeta fursa nyingi kwa wananchi wetu,” amesema Waziri Jafo. Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK, ameeleza kuwa JTC ni jukwaa muhimu litakalosaidia kuondoa vikwazo vya kibiashara, kurahisisha michakato ya biashara na kuvutia uwekezaji mpya. “Kamati ya Pamoja ya Biashara itakuwa jukwaa lenye nguvu la kuondoa vikwazo, kukuza uwekezaji, na kufungua fursa mpya kwa mataifa yote mawili,” ameeleza Balozi Goktug. Ameongeza kuwa Uturuki imejipanga kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu, kilimo, nishati na teknolojia, huku akisisitiza dhamira ya kuimarisha maendeleo ya pamoja chini ya uongozi wa Rais Erdoğan na Rais Samia. Kwa ujumla, Tanzania ina matumaini makubwa kuwa ushirikiano huu utafungua ukurasa mpya wa maendeleo ya kiuchumi, ajira na mafanikio kwa wananchi wake. Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hafla ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki iliyofanyika leo Julai 23,2025 jijini Dar es Salaam. Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK,wakati wa hafla ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki iliyofanyika leo Julai 23,2025 jijini Dar es Salaam.

Articles similaires

WAZIRI MAVUNDE AKAGUA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA NANE LA MAFUNZO YA UONGEZAJI THAMANI MADINI VITO

msumbanews.co.tz - 22/Jul 15:26

  ▪️Bilioni 33 kukutumika kukamilisha Jengo la ghorofa pacha-TGC Arusha▪️Biashara ya madini kufanyika kwenye Jengo▪️Ni mkakati wa...

TANZANIA NA KENYA WAZINDUA RASMI MAUNGANISHO YA MKONGO WA MAWASILIANO

msumbanews.co.tz - 18/Jul 16:38

Mawaziri wa Mawasiliano kutoka Tanzania na Kenya wamezindua rasmi maunganisho ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) wa Tanzania unaosimamiwa na...

TANZANIA NA KENYA WAZINDUA RASMI MAUNGANISHO YA MKONGO WA MAWASILIANO

msumbanews.co.tz - 18/Jul 16:38

Mawaziri wa Mawasiliano kutoka Tanzania na Kenya wamezindua rasmi maunganisho ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) wa Tanzania unaosimamiwa na...

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ASHIRIKI KIKAO CHA KIMATAIFA CHA SHERIA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI

msumbanews.co.tz - 22/Jul 13:19

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari ameshiriki kikao cha 58 cha Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Sheria za Biashara na Uwekezaji...

WASHIRIKA WA MAENDELEO KUCHANGIA SH. BILIONI 161 MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

msumbanews.co.tz - 19/Jul 06:26

 Na. Peter Haule, WF, Dar es SalaamSerikali ya Tanzania na washirika wa Maendeleo wanaochangia Mfuko wa Afya wa Pamoja (Health Basket Fund),...

WASHIRIKA WA MAENDELEO KUCHANGIA SH. BILIONI 161 MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

msumbanews.co.tz - 19/Jul 06:26

 Na. Peter Haule, WF, Dar es SalaamSerikali ya Tanzania na washirika wa Maendeleo wanaochangia Mfuko wa Afya wa Pamoja (Health Basket Fund),...

MAFUNZO YA UIMARISHAJI MPAKA WA KIMATAIFA KUWAJENGEA UELEWA WATAALAMU WA TANZANIA NA BURUNDI

msumbanews.co.tz - 22/Jul 15:48

 Na Munir Shemweta, WANMM Serikali imesema kuwa, mafunzo ya uimarishaji mpaka wa kimataifa kati ya Tanzania na Burundi yanalenga kujenga uelewa wa...

AIRTEL YAZINDUA HUDUMA YA ‘AIRTEL CHAPAKAZI’ MAALUM KWA WAJASIRIAMALI

msumbanews.co.tz - 16/Jul 17:16

 Airtel Tanzania leo imezindua rasmi huduma ya Airtel Chapakazi, suluhusho jipya lililoundwa kuchochea ukuaji wa wajasiriamali na wafanyabiashara...

AIRTEL YAZINDUA HUDUMA YA ‘AIRTEL CHAPAKAZI’ MAALUM KWA WAJASIRIAMALI

msumbanews.co.tz - 16/Jul 17:16

 Airtel Tanzania leo imezindua rasmi huduma ya Airtel Chapakazi, suluhusho jipya lililoundwa kuchochea ukuaji wa wajasiriamali na wafanyabiashara...

MAKUBALIANO MAPYA YA ATCL NA KENYA AIRWAYS KUINUA VIWANGO VYA HUDUMA ZA ANGA

msumbanews.co.tz - 28/Jul 18:22

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAMSHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL) wamesaini mkataba wa makubaliano na Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways)...

Les derniers communiqués

  • Aucun élément