X

Vous n'êtes pas connecté

Rubriques :

  - MSUMBANEWS.CO.TZ - A La Une - 19/Jul 06:42

MD TWANGE AKAGUA MAENDELEO YA MIRADI YA UMEME DODOMA

 Awataka Wakandarasi kuongeza kasi ili Miradi ikamilike kwa wakatiAsema lengo la TANESCO ni kuhakikisha inamudu mahitaji ya wateja wakeMkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange Julai 18, 2025 amefanya ziara ya kuagua maendeleo ya Miradi ya umeme ukiwemo wa Njia ya kusafirisha umeme kutoka Zuzu hadi Mbande, Mradi wa kusambaza umeme ardhini katika mji Serikali na Mradi wa Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mjini Mkoani Dodoma.Bw. Twange ameelezea maendeleo ya  Mradi wa njia ya kusambaza umeme wa Msongo wa Kilovolti 33 kutoka Mbande hadi Zuzu  kwamba umefikia asilimia 48.35 huku Mradi wa usambazaji wa umeme ardhini kwenye mji wa Serikali Ihumwa ukifikia asilimia 64 ambapo hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 50.09 ambapo amewataka Wakandarasi kuongeza kasi ili Miradi hiyo ikamilike kwa wakati na ianze kuwahudumia wananchi.Mkurugenzi Mtendaji huyo pia amekagua maendeleo ya Mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mjini Dodoma ambacho kimefikia zaidi ya asilimia 80 na  kinatarajia kukamilika rasmi mwanzoni mwa mwezi Septemba Mwaka huu.‘’Kituo cha kupokea umeme cha mjini kimefikia zaidi ya asilimia 80, nataka kuwaeleza kuwa mwanzoni mwa mwezi wa tisa Kituo  hiki kitakamilika. Kituo hiki kitatupa uwezo wa kuwasambazia umeme wateja wetu walioko Katikati ya mji  kwa kuwa kituo kilichokuwepo awali kilizidiwa na  tunachotaka ni kumudu mahitaji ya wateja wetu, alifafanua Bw. Twange.Aidha, Bw. Twange amesema licha ya changamoto za kifedha zilizojitokeza kwa baadhi ya miradi  amewapongeza wasimamizi wa Miradi kutoka TANESCO na Wakandarasi ambapo ameeleza kuwa kukamailika kwa miradi hiyo  kutachangia upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa  Mkoa wa Dodoma na maeneo Jirani ya Mkoa wa Morogoro.

Articles similaires

MD TWANGE AKAGUA MAENDELEO YA MIRADI YA UMEME DODOMA

msumbanews.co.tz - 19/Jul 06:42

 Awataka Wakandarasi kuongeza kasi ili Miradi ikamilike kwa wakatiAsema lengo la TANESCO ni kuhakikisha inamudu mahitaji ya wateja wakeMkurugenzi...

MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA (EACOP) UMELETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI KWA WANANCHI WA TANGA

msumbanews.co.tz - 16/Jul 17:03

 📌Wananchi wampongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mafanikio ya ujenzi wa Mradi, wafikia...

MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA (EACOP) UMELETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI KWA WANANCHI WA TANGA

msumbanews.co.tz - 16/Jul 17:03

 📌Wananchi wampongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mafanikio ya ujenzi wa Mradi, wafikia...

JIKO LA UMEME LATULIZA NDOA KIJIJI CHA MAENDELEO MOSHI

msumbanews.co.tz - 24/Jul 05:34

Afisa Uhusiano ,Huduma kwa Wateja wa Shirika la Umeme (TANESCO) mkoa wa Kilimanjaro Bi Mwanaisha Mbita akikabidhji jiko la umeme kwa familia ya...

JIKO LA UMEME LATULIZA NDOA KIJIJI CHA MAENDELEO MOSHI

msumbanews.co.tz - 24/Jul 05:34

Afisa Uhusiano ,Huduma kwa Wateja wa Shirika la Umeme (TANESCO) mkoa wa Kilimanjaro Bi Mwanaisha Mbita akikabidhji jiko la umeme kwa familia ya...

KATIBU MKUU MKOMI AKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA UJENZI WA MAKAZI YA WATUMISHI KIJIJI CHA KIJIWENI

msumbanews.co.tz - 15:16

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wakwanza kushoto) akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya...

WIZARA ZINGINE ZIIGE MFANO WA WIZARA YA AFYA KUHAMIA MTUMBA- LUKUVI

msumbanews.co.tz - 23/Jul 17:55

 Na WAF - Dodoma Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi ameipongeza Wizara ya Afya kwa kuchukua uamuzi wa...

WAZIRI MAVUNDE AKAGUA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA NANE LA MAFUNZO YA UONGEZAJI THAMANI MADINI VITO

msumbanews.co.tz - 22/Jul 15:26

  ▪️Bilioni 33 kukutumika kukamilisha Jengo la ghorofa pacha-TGC Arusha▪️Biashara ya madini kufanyika kwenye Jengo▪️Ni mkakati wa...

VITUO VIWILI VYA KUPUNGUZA KASI YA MAFUTA GHAFI EACOP KUJENGWA NCHINI

msumbanews.co.tz - 24/Jul 05:46

 📌Vinalenga kupunguza kasi ya Mafuta kutoka Hoima Uganda hadi Chongoleani Tanzania📌Ujenzi wafikia asilimia 50📌 Mabomba ya kipenyo cha inchi...

VITUO VIWILI VYA KUPUNGUZA KASI YA MAFUTA GHAFI EACOP KUJENGWA NCHINI

msumbanews.co.tz - 24/Jul 05:46

 📌Vinalenga kupunguza kasi ya Mafuta kutoka Hoima Uganda hadi Chongoleani Tanzania📌Ujenzi wafikia asilimia 50📌 Mabomba ya kipenyo cha inchi...

Les derniers communiqués

  • Aucun élément