Na. Eva Ngowi -Wizara ya Fedha, Dar es Salaam Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar...
Vous n'êtes pas connecté
*Na Mwandishi wetu- RUKWAMkuu wa Wilaya ya Sumbawanga na Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Wilaya, Mhe. Nyakia Ally Chirukile, amezindua rasmi mafunzo ya usimamizi wa maafa kwa wajumbe wa kamati za wilaya hiyo, akisisitiza umuhimu wa kuwa tayari kabla ya majanga kutokea.Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, yaliyofanyika tarehe 21 Julai, 2025 kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Idara ya Menejimenti ya Maafa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Mhe. Chirukile amesema kuwa maafa kama maporomoko ya ardhi, mlipuko wa kipindupindu, radi na ajali za majini yameathiri jamii na uchumi wa wilaya hiyo.> “Kuchukua hatua kabla ya majanga ni nafuu zaidi kuliko kushughulika na athari. Mafunzo haya ni nyenzo ya kuongeza ufanisi wetu katika kuzuia na kukabili majanga,” alisema Mhe. Chirukile.Kwa upande wake, Kanali Selestine Masalamado kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Idara ya Maafa, amesema mafunzo hayo ni utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022, na yana lengo la kuwawezesha viongozi wa serikali za mitaa kuwa mstari wa mbele wakati wa dharura. Naye mwakilishi wa UNDP, Bi. Clara Peter Maliwa, amepongeza Wilaya ya Sumbawanga kwa kujitoa kikamilifu kushiriki mafunzo hayo na ameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha mifumo ya kukabili majanga nchini.Mafunzo haya yamewaleta pamoja wajumbe wa Kamati Elekezi ya Maafa ya Wilaya na Kamati ya Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, wakiwa na lengo la kujifunza mbinu bora za kupanga, kukabili, na kurejesha hali baada ya majanga.
Na. Eva Ngowi -Wizara ya Fedha, Dar es Salaam Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar...
Na. Eva Ngowi -Wizara ya Fedha, Dar es Salaam Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar...
Na.Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Mhe. Hussain Bashe, amesema wadau wote wa zao la tumbaku watakaoshindwa kushiriki katika zoezi la usajili wa...
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari,akizungumza leo Oktoba 7, 2025, jijini Dodoma, wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili...
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba, ametoa wito kwa wajumbe wa Baraza jipya la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na...
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba, ametoa wito kwa wajumbe wa Baraza jipya la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na...
Serikali kupitia Wizara ya Fedha, imefanya kikao kazi cha Mapitio ya Matumizi ya Fedha za Umma, (Public Expenditure Review -PER) ngazi ya sekta,...
Na Mwandishi Wetu, ArushaWiki ya mafunzo maalum kwa wataalamu wanaotumia vifaa vya ukaguzi wa mizigo (Baggage Scanners) imehitimishwa kwa mafanikio...
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kupitia Shamba la Miti la Sao Hill, limeanza kutumia teknolojia mpya za kidigitali kuboresha utambuzi na...
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali imefanikiwa kutoa kiasi cha shilingi trilioni 3.5 kufikia mwaka 2024 kwa ajili ya uwezeshaji wa...