WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mb) amezitaka Taasisi za Umma ambazo bado...
Vous n'êtes pas connecté
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akiwa ameongozana na wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo mara baada ya kuwasili katika Kijiji hicho alipofanya ziara iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyevaa miwani) akisisitiza jambo kwa Viongozi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati Waziri huyo alipofanya ziara iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyenyanyua mikono) akielekeza jambo kwenye korongo linalohitaji kujengwa daraja katika Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na Wananchi na Viongozi mara baada ya kuwasili katika Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Mwenyekiti Mstaafu wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo Bi. Grace Ndogwe akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa ziara ya Waziri huyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Wananchi na Viongozi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo wakati akisalimiana na Wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo mara baada ya kuwasili wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Na. Mwandishi Wetu-ChipogoloWaziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ametoa wito kwa wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa kushiriki shughuli za maendeleo katika kijiji hicho.Mhe. Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ametoa kauli hiyo tarehe 25 Februari, 20245 akiwa kwenye ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Kata hiyo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.Akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Chamsisili, Mhe Simbachawene amewasisitiza wananchi wa Kijiji hicho kuweka nguvu kazi kubwa kwenye daraja wanalokusudia kujenga kufuatia korongo kubwa lililoko sehemu ya Kijiji hicho.Naomba mshiriki maendeleo katika Kata yenu, adha tunayoipata kwa kutokushiriki maendeleo ni kubwa, hivyo tujitahidi kutumia nguvu zetu wakati Serikali inatafuta namna ya kufanya kupitia taasisi yake ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA). Amesisitiza Waziri Simbachawene.Katika kuhakikisha ujenzi wa daraja hilo unatekelezwa kwa haraka, Waziri Simbachawene ameahidi kuchangia mifuko 300 ya saruji. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kufanya ziara hiyo ambayo italeta chachu kwa maendeleo ya Kata hiyo.Vilevile Mhe. Mwanika amempongeza Waziri Simbachawene kwa ahadi ya mifuko 300 ya saruji itakayoongeza nguvu kubwa katika kukamilisha daraja hilo na kuahidi kushirikiana nae pamoja na wananchi wa Kijiji hicho kwa lengo la kuleta maendeleo.
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mb) amezitaka Taasisi za Umma ambazo bado...
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema zaidi ya asilimia 40 ya Watumishi...
Atakagua na Kuzindua Miradi ya MaendeleoWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu -Mhe. Ridhiwani Kikwete leo...
...... Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe Dkt. Selemani Jafo (Mb.) ameliagiza Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kukamilisha majadiliano na...
Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha za miradiWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi , Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani...
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imempongeza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe....
📌 Ni katika ziara ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Tanga📌Vijiji vyote 118 vyafikishiwa umemeWananchi wa Wilaya ya Korogwe wameipongeza...
Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe Victoria Mwanziva anaendelea na ziara maalum ya kata kwa kata kwa malengo ya ukaguzi wa miradi sambamba na kusikiliza na...
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango...
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amemshukuru Rais wa...