Mkurugenzi wa Ufundi na Undelezaji kutoka Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL,Mhandisi Cecil Francis ameeleza kuwa wamefanikiwa kuunganisha wilaya...
Vous n'êtes pas connecté
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa Ziara ya Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi alipotembelea kituo cha Mkongo wa Baharini cha 2 Africa.Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi akimsikiliza Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano alipotembea mkongo wa Baharini uliopo Mbezi Beach Tangibovu jijini Dar es Salaam.SERIKALI imesema Kipaumbele chake ni kuona idadi ya watumiaji wa data inaongezeka katika jamii ya Watanzania.Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi wakati alipotembelea Airtel Tanzania na mkongo wa Baharini wa 2 Africa uliopo Mbezi Beach Tangibovu jijini Dar es Salaam leo Agosti 09, 2024. Amesema kuwa kwa sasa watu wachache wamefikiwa na matumizi ya data.Amesema ili matumizi ya mkongo wa Baharini uwe mkubwa lazima simu janja ziwafikie watu wengi zaidi hadi vijijini."Watanzania wakishaweza kupata simu janja hizi kwa gharama nafuu basii matumizi ya mkongo huu wa baharini utakuwa ni makubwa zaidi." Amesema Mhandisi MarypriscaAmesema manufaa zaidi yataonekana na vilevile kituo cha Airtel kitandelea kuwa Cha manufaa zaidi kwasababu watumiaji nao watakuwa wameongezeka kila iitwapo leo.Pia imetoa wito kwa wadau mbalimbali ambao waweza kuingiza simu janja kwa gharama nafuu ili Kila mmoja aweza kupata na kuongeza matumizi ya mkongo wa 2 Africa yaweze kuwa makubwa zaidi.Amesema serikali inatoa ushirikiano mkubwa ambao unawezesha kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi."Kama hapo zamani walikuwa wanatumia 2G kwamana watu walikuwa wanaweza kupata tu sauti kwahio Sasa wamekuja kuupgrade kwa 3G paka 5G kwalengo la kuboresha matumizi ya data Kama wananchi wanaweza kutumia intaneti kwa wingi lakini vilevile wanaweza kuboresha maisha na kuwa ya kidijitali zaidi." Ameeleza Mhandisi MarypriscaKwa upande wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano amefurahishwa na ziara ya naibu waziri Maryprisca Mahundi kutembelea Airtel Kama kampuni ya simu za mkononi."Ziara yake ilianzia hapa kwenye mkongo wa baharini wa 2 Africa Kama mnvyofahamu ni kwamba huu mkongo ambao ulizinduliwa na Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan mwaka jana mwezi wa nane sisi kwetu ni fahari kubwa Sana kwasababu mkongo huu unaunganisha mabara matatu nikimaanisha Afrika, Asia na Europe lakini vilevile una ukubwa wa km zaid ya 45 elfu." AmelezaAmesema kuwa mkongo huu utaisaidia Tanzania kwa kuifungua na kumekuwa na mikakati mingi pia wanakukaribisha wawekezaje kuja nchini kwani miundombinu hiyo ni muhimu sana na inatoa mawasiliano lakini pia inaunganisha mabara mbalimbali.Pia amewakaribisha wadau wote wa mawasiliano kwenda kununua 'capacity' uwezo kutoka kwenye kituo mkongo wa baharini wa 2 Africa kilichopo Mbezi Beach Tangibovu jijini Dar Es Salaam.
Mkurugenzi wa Ufundi na Undelezaji kutoka Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL,Mhandisi Cecil Francis ameeleza kuwa wamefanikiwa kuunganisha wilaya...
Kampuni ya simu za mkononi Airtel kupitia kwa Mkurugenzi wa Biashara Joseph Muhele amesema kuwa mtandao huo mwaka huu 2024 unaendelea kufangua...
Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb), amewataka viongozi wa Mfuko wa Mawasiliano...
Naibu Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amehitimisha ziara yake ya siku tatu kutembelea...
Naibu Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amehitimisha ziara yake ya siku tatu kutembelea...
Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi MaryPrisca Mahundi (Mb), ametembelea Ofisi za Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote...
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezitaka Mamlaka za Udhibiti na Ununuzi wa Umma Afrika Mashariki kuzingatia weledi,...
Tanzania ina mifumo kadhaa ya kisheria na udhibiti inayoongoza sekta ya mawasiliano na TEHAMA ili kuhakikisha huduma ya intaneti ya kasi inawafikia...
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amezitaka Hospitali zote nchini kuanzisha mfumo wa matumizi ya simu za upepo ili kupunguza matumizi ya siku za...
KUPITIA Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) inatekeleza mradi wa EASTRIP (East Africa Skills for...