KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imepongeza juhudi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika kuboresha mitaala yake ili kukidhi...
Vous n'êtes pas connecté
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo Husna Sekiboko ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh. Dkt. Samia Suluhu Hssan kwa uamuzi wake wa kujenga ofisi na maabara za Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Zanzibar jambo litakalosaidia upimaji wa sampuli mbalimbali pamoja na kusaidia watafiti kuitumia maabara hiyo.SEKIBOKO ameyasema hayo baada ya ziara ya kamati ya kudumu ya bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo kutembelea ofisi na maabara za TAEC eneo la Dunga Zuze Zanzibar ambapo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 100 kwa sasa usimikaji wa miundombinu pamoja na ununuzi wa vifaa vya maabara unaendelea.Kwa upande wake Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mh. Omary Kipanga amesema katika mchakato wa uzalishaji bidhaa pamoja na chakula suala la mionzi haliwezi kuepukika kwa kuwa vyakula vinavyoingizwa ndani ya nchi na vinavyotoka nje ya nchi ni lazima viratibiwe vizuri ili visiwe na athari za mionzi hivyo uwepo wa maabara ya upimaji wa mionzi Zanzibar kunaimarisha usalama wa wananchi pamoja na mazingira .Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Prof. Najat Kassim Mohammed amesema ofisi na maabara za TAEC Zanzibar zimejengwa eneo maalum la kimkakati la viwanda hivyo bidhaa zinazohitaji kupimwa mionzi zitapimwa katika maabara hiyo jambo litakalorahisisha utendaji.Kamati ya kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo inetembelea miradi mbalimbali ya kimkakati nchini kwa lengo la kuona namna fedha zinazotolewa na serikali baada ya kupitishwa na bunge zinavyotumika kwa maslahi ya taifa.
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imepongeza juhudi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika kuboresha mitaala yake ili kukidhi...
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Prof. Najat Kassim Mohamed amesema Taasisi hiyo itakuwa mlezi wa programu maalumu ya...
Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Michael Ng’umbi akitoa maelezo ya utekelezaji wa Mradi wa kuimarisha ubora wa elimu ya...
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Fatuma Toufiq akizungumza wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua...
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla akizungumza na Wahariri pamoja na Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali, Septemba...
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla akizungumza na Wahariri pamoja na Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali, Septemba...
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Ahmed Abbas Ahmed ,akizungumza na wamiliki wa hoteli kuhusu fursa za Tamasha la Kitaifa la Utamaduni Baadhi ya wamiliki wa...
Serikali imezitaka Kamati za Usimamizi wa Maafa Ngazi ya Wilaya kuhakikisha zinajiandaa kikamilifu na kuweka mpango wa dharula wa utendaji na uratibu...
Serikali imezitaka Kamati za Usimamizi wa Maafa Ngazi ya Wilaya kuhakikisha zinajiandaa kikamilifu na kuweka mpango wa dharula wa utendaji na uratibu...
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ikiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb)imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa...