Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezitaka Mamlaka za Udhibiti na Ununuzi wa Umma Afrika Mashariki kuzingatia weledi,...
Vous n'êtes pas connecté
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amezitaka Hospitali zote nchini kuanzisha mfumo wa matumizi ya simu za upepo ili kupunguza matumizi ya siku za mkononi ambazo hazina tija kwenye utoaji wa huduma bora kwa wananchi.Waziri Mhagama ameyasema hayo leo Septemba 12, 2024 jijini dodoma wakati wa uzinduzi wa miradi na matukio katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.Amesema simu hizo zitasaidia uwajibikaji wa watumishi wa sekta ya afya na kugundua utoro kwa watumishi wasiohudhuria kazini.“Mfumo huu ni mzuri sana hongereni kwa ubunifu nitumie fursa hii kuagiza hospitali zote nchini kuanzisha na kutumia mfumo huu ambao utasaidia kubaini utoro kwa watumishi”Waziri Mhagama ameupongeza uongozi wa Hospitali hiyo kwa ubunifu huo mzuri na utoaji wa huduma bora kwa wateja kupitia mbinu za kuhakikisha wanawahudumia wagonjwa kwa ufanisi na kuleta tija.Wakati huo huo.Mhe. Mhagama amesema kuwa Magari matatu ya upasuaji aliyoyazindua yanalengo la kutoa huduma za kibingwa za upasuaji kwa watanzania hususan ni hospitali zilizopo pembezoni mwa nchi ambazo hazina vyumba vya kufanyia huduma husika.“Magari haya yatatumika kwa miezi mitatu yatasaidia kuwafikia wananchi wengi ambao wako katika maeneo yasiyo na vyumba vya upasuaji na kuondoa gharama za matibabu na kutoa mafunzo katika hospitali hizo magari hayo yataweza kuimarisha tiba utalii na kuitangaza Tanzania.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezitaka Mamlaka za Udhibiti na Ununuzi wa Umma Afrika Mashariki kuzingatia weledi,...
NAIBU waziri mkuu Dk Dotto Biteko amewataka maafisa manunuzi na ugavi nchini kufanya kazi zao Kwa uadilifu ,uwajibikaji uwazi na maadili katika...
Na Veronica Simba, WMA DodomaWakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Dodoma imetoa elimu ya vipimo kwa Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa...
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde akizungumza wakati akizindua chama cha Wasambazaji wa Sekta ya Madini Tanzania (TAMISA) jiji Dar es...
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde akizungumza wakati akizindua chama cha Wasambazaji wa Sekta ya Madini Tanzania (TAMISA) jiji Dar es...
Serikali imesema kuwa itaanza kuchukua hatua kwa wahudumu wa afya watakaobainika kuzembea katika usafi na kusababisha mashuka ya vitanda vya wagonjwa...
Serikali imesema kuwa itaanza kuchukua hatua kwa wahudumu wa afya watakaobainika kuzembea katika usafi na kusababisha mashuka ya vitanda vya wagonjwa...
Wajasiriamali wadogo wapatao 500 wanaojihusisha na uchimbaji na uchakataji kokoto Jijini Dar es Salaam wamewezeshwa vifaa kinga na kupatiwa mafunzo...
Wajasiriamali wadogo wapatao 500 wanaojihusisha na uchimbaji na uchakataji kokoto Jijini Dar es Salaam wamewezeshwa vifaa kinga na kupatiwa mafunzo...
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla akizungumza na Wahariri pamoja na Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali, Septemba...