X

Vous n'êtes pas connecté

Rubriques :

Maroc Maroc - MSUMBANEWS.CO.TZ - A La Une - 13/Sep 05:26

HAKIELIMU YAZINDUA MRADI WA MAJARIBIO KUWEZESHA WALIMU KUFUNDISHA KWA VITENDO

 Shirika la HakiElimu Tanzania limezindua mradi wa majaribio ambao umelenga kukuza ufundishaji wa walimu,kupitia teknolojia ambayo itamwezesha Mwanafunzi kupata picha halisi ya kitu anachofundishwa.Akizungumza leo Septemba 12,2024 Jijini Dar es salaam Mkuu wa Programu Shirika la HakiElimu Bw.Godfrey Boniventura wakati wa uzinduzi wa mradi huo amesema kuwa mradi huo umekusudia kumfundisha mwanafunzi kwa vitendo na sio nadharia pekee ambapo wanafunzi watafundishwa kwa kutumia vitu katika picha na maumbo yake halisi."Hata kama unataka kumfundisha mtu awe makenika (fundi wa gari) labda kufunga mguu wa gari(shock up) unamfundisha kwa maumbo halisi na kumuonesha inapofungwa ambapo anapata picha halisi kwa namna ya kufanya". Amesema.Aidha Boniventura amesema baada ya mradi huo wa majaribio kukamilika wanatarajia kutanua wigo kwa kushirikisha taasisi mbalimbali za elimu nchini.Aidha Boniventura amesema Taasisi ya Hamk ,Save the Children na taasisi 5 za kitaaluma zimeshiriki katika kuhakikisha utekelezaji mzuri wa mradi huo wa majaribio ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ambapo itakuwa njia nzuri ya kupima ufanisi na umuhimu wake katika mazingira ya Kitanzania.Kwa upande wake kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Dkt. Abdalah Ngodu ametoa shukrani zake kwa waandaaji wa mradi huo ambapo anatarajia kuona ubunifu na mipango yenye matokeo kwenye maisha ya wanafunzi kwa kuzalisha ujuzi wenye kuleta tija kwa jamii.Aidha amesema kuwa ukuaji wa kasi wa teknolojia,unachangia uhitaji wa zana za kisasa kama teknolojia ya VR na XR ambao pia ni sehemu ya maudhui ya mradi huo ambapo inatoa mwanya kwa wakufunzi na wanafunzi kujifunza mtandaoni kwa pamoja kabla ya kufanya vitendo katika ulimwengu halisi.Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mafunzo ya Amali (VTA), Dkt. Bakari Ali Silima amesema uingizwaji wa mfumo wa kidijitali wa maudhui ya mafunzo katika teknolojia ya vipimo vitatu na matumizi ya miundombinu ya TEHAMA, kutawezesha kutumia mwalimu mmoja kutoa mafunzo kwa wanafunzi wengi katika maeneo tofauti kwa wakati mmoja.Mradi huo wa majaribio unatarajiwa kufanyika kwa miaka miwili ambapo umefadhiliwa na kampuni ya 3D BEAR na kuratibiwa nchini na Chuo kikuu Cha Hamk,Shirika la Save The Children,HakiElimu pamoja na vyuo vikuu Vitano.

Articles similaires

TAEC KUSHIRIKIANA NA ATC KUTOA STASHAHADA YA NYUKLIA

msumbanews.co.tz - 07:44

 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Prof. Najat Kassim Mohamed amesema Taasisi hiyo itakuwa mlezi wa programu maalumu ya...

DKT. BITEKO ASISITIZA MAADILI, WELEDI NA UWAJIBIKAJI KATIKA UNUNUZI WA UMMA

msumbanews.co.tz - 09/Sep 13:54

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezitaka Mamlaka za Udhibiti na Ununuzi wa Umma Afrika Mashariki kuzingatia weledi,...

MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO WIZARA YA ELIMU ATEMBELEA MRADI WA EASTRIP, NIT

msumbanews.co.tz - 14/Sep 05:06

 KUPITIA Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) inatekeleza mradi wa EASTRIP (East Africa Skills for...

Waziri Bashungwa ataka Wahandisi kulinda thamani yao

msumbanews.co.tz - 06/Sep 04:54

 Waziri wa Ujenzi,Innocent Bashungwa amewataka Wahandisi kuwajibika katika majukumu pale wanapopatiwa mradi ili kulinda thamani yao. Akizungumza...

Kamati ya Bunge Yaipongeza UDSM kwa Maboresho ya Mitaala na Utekelezaji wa Mradi wa HEET

msumbanews.co.tz - 11/Sep 04:51

 KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imepongeza juhudi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika kuboresha mitaala yake ili kukidhi...

Naibu waziri Mkuu Amewataka Maafisa manunuzi na ugavi nchini kufanya kazi Kwa uadilifu ,uwajibikaji na uwazi

msumbanews.co.tz - 10/Sep 18:08

NAIBU waziri mkuu Dk Dotto Biteko amewataka maafisa manunuzi na ugavi nchini kufanya kazi zao Kwa uadilifu ,uwajibikaji uwazi na maadili katika...

OSHA YAWAWEZESHA WACHIMBAJI, WAPONDAJI KOKOTO DAR ES SALAAM

msumbanews.co.tz - 15/Sep 05:02

 Wajasiriamali wadogo wapatao 500 wanaojihusisha na uchimbaji na uchakataji kokoto Jijini Dar es Salaam wamewezeshwa vifaa kinga na kupatiwa mafunzo...

OSHA YAWAWEZESHA WACHIMBAJI, WAPONDAJI KOKOTO DAR ES SALAAM

msumbanews.co.tz - 15/Sep 05:02

 Wajasiriamali wadogo wapatao 500 wanaojihusisha na uchimbaji na uchakataji kokoto Jijini Dar es Salaam wamewezeshwa vifaa kinga na kupatiwa mafunzo...

HAKI ELIMU : VIJANA WENGI WA SEKONDARI HAWANA UELEWA NA DEMOKRASIA

msumbanews.co.tz - 11/Sep 06:30

Mkuu wa Idara ya Utafiti kutoka Haki Elimu Makumba Mwemezi amesema utafiti uliofanywa na Taasisi hiyo umebaini kuwa asilimia 44.4 ya vijana katika...

AIRTEL TANZANIA YAENDELEA KUPANUA WIGO VIJIJINI

msumbanews.co.tz - 06:15

Kampuni ya simu za mkononi Airtel kupitia kwa Mkurugenzi wa Biashara Joseph Muhele amesema kuwa mtandao huo mwaka huu 2024 unaendelea kufangua...

Les derniers communiqués

  • Aucun élément