X

Vous n'êtes pas connecté

Rubriques :

Maroc Maroc - MSUMBANEWS.CO.TZ - A La Une - 04/Sep 13:38

WMA YAHIMIZA MATUMIZI YA MIZANI ILIYOHAKIKIWA KWA WAFANYABIASHARA WA GESI

  Na Pendo Magambo – WMA, Dar es SalaamWakala wa Vipimo Tanzania (WMA) imewataka wafanyabiashara wa gesi kutumia mizani iliyohakikiwa na WMA ili kujiridhisha na usahihi wa uzito wa mitungi ya gesi kabla ya kuiuza kwa wateja.Wito huo ulitolewa Septemba 3, 2024 jijini Dar es Salaam na Afisa Vipimo Yahya Tunda kutoka WMA Mkoa wa kivipimo Ilala, wakati wa semina jumuishi iliyoandaliwa na kampuni ya Gesi ya Oryx kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wote.Tunda alieleza kuwa WMA inatekeleza majukumu yake kupitia Sheria ya Vipimo sura namba 340, ambayo inasimamia matumizi ya vipimo sahihi na kwa upande wa wafanyabiashara wanaotumia mizani, sheria inawataka kutumia zile zilizohakikiwa na WMA ili kuleta usawa wa kivipimo kwenye maeneo ya biashara, afya, usalama na mazingira.“Ninawashauri wafanyabiashara pindi wanapotaka kununua mizani kufika katika ofisi zetu ili wapate ushauri wa kitaalamu kuhusu aina inayofaa kulingana na biashara wanazofanya,” alisisitiza.Akizungumzia kuhusu mizani inayotumiwa na wafanyabiashara kuhakiki uzito wa bidhaa, Tunda alisema kuwa sheria inaelekeza kuweka kibandiko kinachoonesha tarehe ambayo mizani ilihakikiwa pamoja na tarehe ya kurudia uhakiki wake.Aidha, aliwataka wafanyabiashara wa gesi walioshiriki semina hiyo kuwa mabalozi kwa wengine.Kwa upande wake, Msimamizi wa kampuni ya Oryx, Wilaya ya Ilala, Evarist Kisaka aliishukuru WMA kwa kuitikia wito na kutoa elimu ya matumizi sahihi ya vipimo kwa wafanyabiashara wa gesi na wadau mbalimbali wa nishati safi ya kupikia.“Waliohudhuria leo wamepata maarifa mengi, nina uhakika wataenda kufanya biashara zao kwa mlengo chanya zaidi maana wamejua faida za kuwa na vipimo sahihi, suala ambalo litawajengea uaminifu kwa wateja,” alisema.Pamoja na jukumu lake la msingi ambalo ni kumlinda mlaji na mfanyabiashara, WMA pia inachagiza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wote kwa kuhakikisha kuwa panakuwa na usawa katika vipimo vya bidhaa hiyo yanayoendana na thamani ya fedha katika biashara husika.

Articles similaires

WMA, TAKUKURU WATEKELEZA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA

msumbanews.co.tz - 09/Sep 07:07

 Na Veronica Simba, WMA DodomaWakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Dodoma imetoa elimu ya vipimo kwa Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa...

WAZIRI JAFO: WIZI WA KUCHEZEA VIPIMO NI KOSA KISHERIA

msumbanews.co.tz - 12/Sep 07:50

 WAZIRI  wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo amehimiza wananchi jijini Mwanza kuzingatia matumizi sahihi ya vipimo kila mara wanapofanya...

WMA YAHIMIZA USHIRIKIANO KUTOKA SEKTA BINAFSI

msumbanews.co.tz - 12/Sep 08:08

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla akizungumza na Wahariri pamoja na Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali, Septemba...

WMA YAHIMIZA USHIRIKIANO KUTOKA SEKTA BINAFSI

msumbanews.co.tz - 12/Sep 08:08

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla akizungumza na Wahariri pamoja na Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali, Septemba...

WMA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA TEHAMA KWA JESHI LA POLISI ILALA

msumbanews.co.tz - 11/Sep 10:54

  Na Mahamudu Jamal, WMAWakala wa Vipimo (WMA) imekabidhi msaada wa vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa Jeshi la Polisi Mkoa...

SERIKALI KUENDELEA KUTEKELEZA MKAKATI WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

msumbanews.co.tz - 17:04

 Naibu Waziri Nishati,  Judith Kapinga amesema Serikali inaendelea kutekeleza mkakati wa nishati safi ya kupikia utakaowafanya watanzania zaidi ya...

REA YAENDELEA KUTEKELEZA DHAMIRA YA RAIS SAMIA KWA VITENDO

msumbanews.co.tz - 09/Sep 07:03

Na Mohamed SaifWakala wa Nishati Vijijini (REA) umeanza kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan la...

WMA kutoa gawio la sh. Bilioni 7.7 mwaka wa Fedha 2025/2026

msumbanews.co.tz - 12/Sep 05:50

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) Alban Kihulla akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari katikq Mkutano mwendelezo ya Mikutano...

DKT. NCHEMBA ATOA WITO KWA NCHI ZA AFRIKA KUHIMIZA MATUMIZA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

msumbanews.co.tz - 18:24

 Na. Benny MwaipajaWaziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ((Mb), ametoa wito kwa nchi za Afrika kutafuta njia na mikakati ya kuboresha...

SERIKALI KUVUTIA WAWEKEZAJI UTAFUTAJI WA MAFUTA NA GESI- DKT. BITEKO

msumbanews.co.tz - 10/Sep 16:13

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali itaendelea kuvutia wawekezaji katika tafiti na uchimbaji wa mafuta na...

Les derniers communiqués

  • Aucun élément